Saturday, January 30, 2016

Gumzo mitandaoni>>>> Rais wa marekani barak Obama Kukimbia kuwahi ndege yake baada ya kutumia muda wake vibaya....

Habari zilizogonga vichwa vya habari duniani ni tukio la Rais wa marekani barak Obama Kukimbia mbio kuwahi ndege baada ya kutumia muda wake vibaya, na kwa mujibu wa taarifa toka state zinasema muda wa ndege ya Rais unapowadia basi huondoka bila kujali Rais yupo au hayupo kwa ajili ya usalama.

Monday, January 25, 2016

SPIKA WA BUNGE AREJEA KUTOKA INDIA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai amerejea kutoka nchini India alikokuwa akifanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Mheshimiwa Ndugai alisema kwa sasa afya yake iko imara kabisa na anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu na Madaktari waliokuwa wakimfanyia uchunguzi Nchini India.
Mhe. Ndugai pia amewashukuru watanzania wote kwa dua na sala zao katika kipindi alichokuwa India ambazo zimemuwezesha kuimarika kwa afya yake na hatimaye kurejea nchini salama.
Mbali na kutoa shukrani hizo Mheshimiwa Ndugai pia amewatakia Watanzania wote kheri na nafaka ya sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.
Sambamba na hilo Mhe Ndugai amewakumbusha pia Waheshimiwa Wabunge kujiandaa na shughuli za Bunge ambazo zinatarajia kuanza hivi karibuni.
Katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere Mhe. Ndugai alilakiwa na Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt Tulia Ackson ambaye aliambatana na Viongozi wengine wa kitaifa akiwemo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Merdad Kaleman, Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura, Mbunge wa Arusha Mjini Mhe. Godbless Lema na Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah.


SOURCE: http://www.parliament.go.tz/news/spika-wa-bunge-arejea-kutoka-india

Bunge Jipya lanoga... Mitazamo tofauti yaibuka.. SOMA HAPA KUPATA MITAZAMO TOFAUTI ILIOTOLEWA MITAANI..

Kesho wabunge wanarudi bungeni kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni bunge jipya kabisa chini ya Spika Mheshimiwa Job Ndugai na Dk. Tulia, Wananchi wengi wakiwa na matizamo tofauti kuhusu bunge jipya kutokana na mabadiliko mbali mbali yaliyotokea ndani ya bunge hilo kutoka lililo pita.

Wengi wamekuwa na mitazamo tofauti wengi wakiwa wanamategemeo kuwa litakuwa na upinzani  mkubwa kutokana na upinzani kuongezeka maradufu, wengine wakipendekeza sheria dhidi ya wabunge na wazembe ziwekwe uzembe huo ulitajwa kuwa ni kulala, kushikana mashati na kujibizana matusi, huku wengine wakisema wanategemea kilekile maana wakina “hela ya Mboga ndio walewale wameingia” hii ni mitazamo tofauti iliotolewa vijiweni siku ya leo ikiwa ni njia mojawapo ya kupata maoni ya wananchi juu ya bunge jipya.

Sunday, January 24, 2016

Hotuba ya Raisi John Pombe Magufuli.... KUIPATA YOTE SOMA HAPA>>>>>>

Hotuba ya Raisi John Pombe Magufuli bado Kitendawili....  

Sasa yapata zaidi ya miezi miwili tokea Raisi wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kuapishwa kuwa Eaisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wananchi wa Tanzania wamekuwa wakifuatilia kwa makini uongozi mpya huku wakiunga mikono jitihada mbalimbali zinazofanywa na viongozi wetu katika kuinuaa jamii yetu, na huku wengine kama sisi tukisubiri kwa hamu hotuba ya raisi wetu, huku tukitegemea itapagwa kama hotuba ile ya Bunge au zaidi.
Labda tunaishi kwa Mazoea ya Raisi mstaafu, na inaweza kuwa ni sahihi Raisi kuto hutubia wananchi kwa zaidi ya kipindi cha miezi miwili lakini ni muhimu wananchi kujua mipango ya Raisi katika serikali na kuangalia matazamio ya baadae. Huu ni ushauri wangu(Kubwa lao) kuwa Raisi ajipange na atoe hotuba tujue mikakati tunayotakiwa kuiunga mkono, inaweza isiwe kila mwezi ila hata baada ya miezi mitatu itapendeza maana si sahihi kila mwezi hotuba itolewe bila kufanyika chochote.
Ni Mtazamo tu...

Saturday, January 23, 2016

Simu ya Raisi yawa gumzo mitandaoni..... Wengi wahusisha na utani wa lile kabilaa... Unajua ni lipi...

Raisi Dk. John Pombe Magufuli ameonekana kujali taifa kuliko yeye baada ya kuonekana akishona nguo yake mwenyewe na pia akijitadi kupunguza wafanyakazi na hata kutumia karatasi za daftari katika nyaraka zake mbali mbali.
Hii imepelekea kumuhusisha na utani wa makabila, pia utumiaji wake wasimu na kushona nguo pina nao umehusika. Utani huu sio kwa dharau na kejeli ila ni utani wa kujenga na kuonyesha upendo kwa raisi wetu baada ya kutuonyesha kuwa hajajilimbikizia.

kaza Buti Raisi wetu.
Hapa kazi tu...