Saturday, November 21, 2015

Sababu za Mwanaume Kuchepuka, Jua akichepuka anamaanisha nini?

Tamaduni za kiafrika zimempa nguvu sana mwanaume katika maisha na jamii kwa ujumla, kitendo hiki kina mpa ujasiri na hata husababisha  kuweza na kutamani kujaribu vitu vingi tu ikiwa kama kuonja ladha ya mwanamke mwingine zaidi ya mpenzi wake ikiwa kama jaribio.
Hali hii inaonekana ni mazoea au ukaidi ila kwa mtazamo wangu ndio Mwanaume alivyoumbwa, ameumbwa akitamani chochote kizuri na kukichukua na ndio maana nirahisi yeye kupata maendeleo binafsi.
Tuchukulie mfano wa jogoo, anaweza pita kwa matetea wote wa jirani pale ambapo jogoo wa jirani ni mdhaifu na hawezi kutetea tetea walio mzunguka, sawa na wanaume, hupita na kudonyoa kwa wanaume wenziwe wasio linda malizao vizuri!, kama vile jogoo hatasahau nyumbani na kutoa chakula kwa kila tetea atakae mpita na mwanaume yuko vile vile(wanaita kuhongwa)...


Bila kusahau jogoo hurudi nyumbani jioni na kutunza wanawe alio waacha kwa mama yao siku nzima bila kujua wamekula nini, pia mwanaume ni sawa sawa maana hajui familia imekula nini bali huleta kidogo kilichobaki baada ya kula na michepuko huku akijisikitikia vingi alivyopoteza.
Maana ya kurudi mwishoni ni kudhirisha upendo mwanaume alionao kwa mwenzi wake ambao hakuupata huko alipopita, na asiporudi ujue upendo uliompa hauna mashiko.
Huyu mzee nuksi!!, hata akifanya yake tutasema anaigiza.

No comments:

Post a Comment